| ||||||||||||||
| ||||||||||||||
|
AINA ZA HATARI / MFIDUO | MADHARA YA PAPO HAPO / DALILI | KINGA | HUDUMA YA KWANZA / UZIMAJI MOTO |
MOTO |
Huwaka. Michanganyiko ya vioevu vyenye vimumunyisho vya kaboni huweza kuwaka (moto). Hutoa moshi (au gesi) wenye kukereketa au wenye sumu ukiwa motoni.
|
Usiwashe moto.
|
Poda, mnyunyizio wa maji, povu, dioksidi kaboni.
|
MLIPUKO |
Mvuke/hewa mahuluti inayolipuka huweza kufanyika inapovuka 77°C.
|
Mfumo funge wa zaidi ya 77°C, uingizaji hewa.
|
Utokeapo moto: poza mapipa, n.k. kwa kunyunyizia maji.
|
MFIDUO |
|
EPUKA MGUSANO WOWOTE! ZUIA UTOKAJI WA UKUNGU! EPUKA MFIDUO KWA WANAWAKE (WAJAWAZITO)!
|
KWA HALI YOYOTE MWONE DAKTARI!
|
Kuvuta pumzi |
Mchomo. Kikohozi. Kuumwa koo. Kuumwa kichwa. Kukosa pumzi. Udhaifu.
|
Kinga kiambo ya utoaji moshi au kupumua.
|
Hewa safi, mapumziko. Mpeleke kwa matibabu.
|
Ngozi |
Wekundu.
|
Glavu za kinga. Mavazi ya kinga.
|
Vua nguo zilizosibikwa. Suuza na kisha safisha ngozi kwa maji na sabuni. Mpeleke kwa matibabu.
|
Macho |
Wekundu. Maumivu.
|
Miwanivuli ya usalama, au kinga ya macho pamoja na kinga ya kupumulia.
|
Kwanza safisha macho vizuri kwa dakika chache (ondoa lenzi mboni kama inawezekana kuziondoa kwa urahisi), kisha mpeleke kwa daktari.
|
Kumeza |
Mchomo. Kuumwa koo. Kichefuchefu. Kutapika.
|
Usile, usinywe wala kuvuta sigara ukiwa kazini.
|
Sukutua kinywa. Umpe maji mengi ya kunywa. Mpeleke kwa daktari.
|
KUSAFISHA MWAGIKO | UFUNGASHAJI / UWEKAJI LEBO | |||||||
Ondoka katika eneo la hatari. Shauriana na mtaalam. Uingizaji hewa. Kusanya kioevu kinachovuja na kilichomwagika katika vyombo vilivyozibwa kadri inavyowezekana. Fyonza kioevu kilichosalia katika mchanga au kifyonzi ajizi na kisha peleka mahala pa usalama. Usiruhusu kemikali hii iingie katika mazingira. (Kinga ya ziada ya binafsi: nguo kamili za usalama pamoja na vifaa vya kupumulia vilivyo toshelevu).
|
Furushi madhubuti; weka furushi linaloweza kuvunjika katika chombo madhubuti kilichofungwa. Usisafirishe pamoja na vyakula au malisho. Ainisho ya EU Alama: T R: 45-46-60-25-48/20/22-52/53 S: 53-45-61 Angalia: [E] Ainisho ya UN Ainisho ya UN ya Hatari: 6.1 Kikundi Ufungashaji cha UN: III | |||||||
HATUA ZA HARAKA | UHIFADHI | |||||||
Kadi ya Dharura ya Usafiri: TEC(R) - 61GT1-III Msimbo wa NFPA: H 2; F 1; R 1; |
Kinachotenganishwa na vyakula na malisho, metali kama alumini au magnesiamu. Kilichofungwa vizuri.
| |||||||
|
|
DATA MUHIMU | |||
HALI MAUMBILE; INAVYOONEKANA: KIOEVU KISICHO RANGI CHENYE HARUFU KALI. KIOEVU KITEKNIKALI: KAHAWIA MANJANO HADI KAHAWIA ILIYOKOLEA. HATARI KWA MWILI: Mvuke huu ni mzito zaidi kuliko hewa na huweza kusafiri ardhini, uwakaji wa mbali unawezekana. HATARI ZA KIKEMIKALI: Dutu hii hutengana inapokanzwa zaidi ya kuchemka na inapochomwa huzalisha mafusho yenye sumu pamoja na bromidi hidrojeni, kloridi hidrojeni. Humenyuka pamoja na alumini, magnesiamu, bati na aloi zake kukiwa na maji. Hushambulia aina fulani za mpira na mipako. VIKOMO VYA MFIDUO WA KAZI (OELS): TLV haifahamiki. MAK: kuingia kupitia kwa ngozi; Aina ya sarakani: 2; Aina inayoleta mabadiliko kwa seli za uzazi: 2 (DFG 2002). |
NJIA ZA MFIDUO: Dutu hii huweza kufyonzwa ndani ya mwili kwa kuvuta pumzi ya mvuke wake, kupitia kwenye ngozi na kwa kumeza. HATARI ZA KUVUTA PUMZI: Ukolezi unaodhuru unaweza kufikiwa haraka sana kutokana na uvukizi wa dutu hii ifikapo 20°C. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MFUPI: Dutu hii inakera macho, ngozi na njia ya upumuaji. Dutu hii huweza kuathiri mfumo mkuu wa neva na mafigo kusababisha kuharibika kwa utendaji. Mfiduo huweza kusababisha kupungua kwa fahamu. ATHARI ZA MFIDUO WA MUDA MREFU AU UNAORUDIWA: Dutu hii huweza kuathiri ini, mapafu, mafigo na makende kusababisha kuharibika kwa utendaji na vidonda vya tishu. Dutu hii ina uwezekano wa kusababisha kansa kwa binadamu. Husababisha kusumisha kwa uzazi na kukua kwa binadamu. | ||
TABIA ZA KIMAUMBILE | |||
Kiwango mchemko (hutengana): 196°C Kiwango myeyuko: 6.7°C Uzito wiani (maji = 1): 2.1 Umumunyifu katika maji: mbaya Kanieneo mvuke, kPa ifikapo 20°C: 0.1 |
Uzito wiani wa mvuke/hewa mahuluti ifikapo 20°C (hewa = 1): 1.01 Kiwango cha kumweka: 77°C Oktanoli/kizigeu mgawo cha maji kwa logi Pow: 2.96 | ||
DATA YA MAZINGIRA | |||
Dutu hii inadhuru kwa viumbe viishivyo majini.
| |||
VIDOKEZO | |||
Kutegemeana na kiasi cha mfiduo, upimaji wa kitibabu wa mara kwa mara pendekeza. Ongezeko la kiimarishaji au kiviza huweza kuathiri tabia ya kitoksini za dutu hii, shauriana na mtaalam. Vimumunyishaji chukuzi vitumikavyo katika misombo ya kibiashara vyaweza kubadilisha tabia za kimaumbile na za kitoksini. Usichukue nguo za kazi nyumbani.
| |||
MAELEZO YA ZIADA | |||
| |||
| |||
© IPCS, CEC 2005 |